logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Karua ashikilia kuwa marehemu Chebukati alivuruga uchaguzi wa 2022

Alipohojiwa katika runinga moja hapa nchini mnamo Februari 26,2025 Karua alisema Marehemu Chebukati alihitalifiana na uchaguzi 2022

image
na Evans Omoto

Yanayojiri27 February 2025 - 12:12

Muhtasari


  • Uchaguzi wa mwaka wa 2022 ulifanyika Agosti 9,ambapo wawaniaji wa kiti cha urais walikuwa ni wanne William Ruto wa UDA,Raila Odinga wa Azimio la Umoja,George Wajakoya wa Roots Party na Wahiga Mwaure wa Agano Party.
  • Tangu uchaguzi huo kufanyika matukio mengi yametokea huku vyama na viongozi kutoka upande wa serikali na upinzani vikishirikiana na wengine kujiondoa kutoka kwa mirengo waliokuwa wakiegemea.

Aliyekuwa mgombea mwenza wa muungano wa Azimio ambaye pia ni kiongozi wa chama cha PLP Martha Karua  anashikilia kuwa marehemu aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alifeli pakubwa katika uchaguzi mkuu wa 2022.

Katika mahojiano kwenye Citizen TV mnamo Februari 26,2025 Karua alisema kuwa aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC marehemu Wafula Chebukati alifeli pakubwa kulinda na kusimamia uchaguzi kwa njia ya haki na ya wazi.

Alifafanua akisema kuwa tukio la Marehemu Chebukati kuwachukua makamishina wawili kamishina Abdi Guliye na Boya Molu dhidi ya wenzake wanne wakiongozwa na Naibu mwenyekiti Juliana Cherera,Francis Wanderi,Irene Masit na Justus Nyang’aya lilionyesha ukiukaji wa uwazi katika mchakato mzima.

Vilevile Bi Karua alieleza kuwa Mahakama pia ilichangia pakubwa kuvuruga uchaguzi huo akisema kuwa maamuzi yake hayakuzingatia uzito wa walalamishi ikizingatiwa kuwa idadi ya makamishina wanne dhidi ya wawili ilikuwa ni idhibati tosha kuwa kulikuwa na dosari katika uchaguzi huo.

Uchaguzi wa mwaka wa 2022 ulifanyika Agosti 9,ambapo wawaniaji wa kiti cha urais walikuwa ni wanne William Ruto wa UDA,Raila Odinga wa Azimio la Umoja,George Wajakoya wa Roots Party na Wahiga Mwaure wa Agano Party.

Baada  ya uchaguzi huo William Ruto alitangazwa mshindi kwa kuzoa kura milioni saba,laki mia moja sabini na sita  mia moja arubaine na moja(7,176,141) ambapo ilikuwa ni asilimia 50.5%, naye Bwana Odinga alipata jumla ya kura milioni sita,laki mia tisa arubaine na mbili,mia tisa na thelathini(6,942,930) ambapo ilikuwa ni asilimia 48.8% kulingana na mujibu wa IEBC.

Tangu uchaguzi huo kufanyika matukio mengi yametokea huku vyama na viongozi kutoka upande wa serikali na upinzani vikishirikiana na wengine kujiondoa kutoka kwa mirengo waliokuwa wakiegemea.

Karua alitangaza kujiondoa katika muungano wa azimio huku aliyekuwa Waziri mkuu bwana Odinga akijenga ukuruba na serikali tawala ya Kenya Kwanza na kuunda serikali  jumuishi(BROAD BASED GOVERNMENT).

Hata hivyo kulingana na kauli za bi Karua alionyesha ari ya kujitosa kwenye debe ifakapo mwaka wa 2027 huku akiendeleza juhudi na jitihada za kujiimarisha na kujenga urafiki na viongozi wengine wanaonekana kuikosoa serikali ya Rais Ruto.

Bi Karua ,Bwana Stephen Kalonzo Musyoka ,Bwana Rigathi Gachagua na Eugine Wamalwa kwa muda wa siku za hivi karibuni wameonekana kujenga urafiki wa kisiasa na kukuwa na azma moja ya kuunda serikali ifikapo 2027.

Jambo ambalo Bi Karua alisema ni kuwa wanafanya juu chini kupata ushawishi wa kutosha na kupata uungwaji mkono kutoka kwa kizazi cha Gen Z ambacho kitakuwa na nguvu katika uchaguzi ujao wa 2027.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved